Kiongozi wa idara ya rasilimali watu Sayyid Hussein Ayubu amesema “Kongamano limehudhuriwa na idadi kubwa ya viongozi wa idara na vitengo vya Atabatu Abbasiyya tukufu, limeshuhudia kujadiliwa mambo mbalimbali ya kiidara na mbinu za kufanya kazi kiidara”.
Akaongeza kuwa, kongamano limejadili mambo mbalimbali yanayohusu wenye shahada katika Ataba tukufu na namna ya kupata shahada za kisekula, amesisitiza kuwa Ataba inajali sekta ya elimu kwa watumishi wake.





