Kwa picha.. Mazingira mbele ya malalo ya Imamu Alkadhim (a.s) katika usiku wa kumbukumbu ya kifo chake

Malalo ya maimamu wawili Aljawadaini (a.s) katika mji wa Kadhimiyya jijini Baghdad, yameshuhudia mamilioni ya waombolezaji kutoka ndani na nje ya Iraq, waliokuja kuomboleza kifo cha Imamu Alkadhim (a.s).

Kumbukumbu ya kifo chake inasadifu siku ya mwezi ishirini na tano Rajabu, idadi kubwa ya waumini imeingia katika mji wa Kadhimiyya, kukiwa na mawakibu nyingi za utoaji wa huduma mbalimbali kwa waombolezaji.

Atabatu Abbasiyya tukufu inatoa huduma kupitia maukibu mbili, moja ipo karibu na malalo takatifu, inagawa maelfu ya sahani za chakula.

Ataba inasaidia kutoa huduma zingine pia, kama vile kuongoza matembezi ya waombolezaji, kutoa huduma za matibabu, usomaji wa Qur’ani na kujibu maswali ya kifiqhi kutoka kwa zuwaru.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: