Mji wa Kadhimiyya umepokea makundi ya zuwaru kutoka ndani na nje ya Iraq, yaliyokuja kuomboleza kumbukumbu ya kifo cha Imamu (a.s) mwezi ishirini na tano Rajabu.
Atabatu Abbasiyya tukufu imefanya kila iwezalo katika kuhudumia zuwaru, kupitia maukibu iliyokuwa inatoa huduma mbalimbali.








