Makundi ya zuwaru yameshiriki katika usomaji wa Dua Kumail mbele ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s)

Ukumbi wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) katika usiku wa Ijumaa ya mwisho wa mwezi wa Rajabu Aswabu, umeshuhudia idadi kubwa ya zuwaru wakishiriki katika usomaji wa Dua Kumail.

Ibada ya kusoma Dua hiyo tukufu imefanywa katika mazingira tulivu, kwa ushiriki wa idadi kubwa ya zuwaru wa malalo ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).

Watumishi wa Atabatu Abbasiyya tukufu, huweka mazingira mazuri ya usomaji wa dua hiyo kila wiki, huandaa vitabu vya dua, sehemu maalum ya kufanyia ibada, kupuliza marashi pamoja na huduma zingine.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: