Waumini wanashiriki usomaji wa dua Nudba mbele ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s)

Haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) asubuhi ya Ijumaa ya mwisho katika mwezi wa Rajabu, imeshuhudia usomaji wa dua Nudba mbele ya kundi kubwa la zuwaru.

Ibada ya usomaji wa dua imefanywa katika mazingira tulivu na kwa ushiriki wa zuwaru wa Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).

Atabatu Abbasiyya tukufu imeandaa mazingira mazuri, imeweka vitabu vya dua, imeandaa sehemu maalum za kufanyia ibada na kutoa huduma za lazima kwa zuwaru.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: