Watumishi wa idara mbili, idara ya kusimamia haram takatifu na idara ya Masayyid, wameweka shada za maua juu ya dirisha la malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), kufuatia kuingia mwezi mtukufu wa Shabani na kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa wajukuu wa Mtume Muhammad (s.a.w.w).
Harakati hiyo ni sehemu ya ratiba ya Atabatu Abbasiyya katika kuadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa Imamu Hussein na watu wa nyumbani kwake (a.s) katika mwezi mtukufu wa Shabani.






