Kitengo cha Dini katika Atabatu Abbasiyya, kimehitimisha semina ya awamu ya pili ya kuwajengea uwezo watumishi wa Atabatu Abbasiyya tukufu.
Msimamizi mkuu wa semina Shekhe Ali Mujaan amesema: “Kitengo kinaendelea kufanya semina za kuwajengea uwezo watumishi wa Ataba tukufu, semina ya pili imefanywa chini ya anuani isemayo (Imamu Mussa bun Jafari –a.s-)”.
Akaongeza kuwa “Semina imedumu kwa muda wa siku kumi, wameshiriki zaidi ya watumishi 300, kulikuwa na wakufunzi bobezi kutoka hauza ya kielimu na shule ya Darul-Ilmi”.
Mujaan akabainisha kuwa “Mada za semina zimejikita katika masomo ya Fiqhi, Aqida na Qur’ani”. Akasema: “Semina imekuwa na matokeo chanya kielimu kwa washiriki”.

