Waumini wameshiriki katika usomaji wa Dua Nnudba mbele ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s)

Ukumbi wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) katika siku ya Ijumaa ya pili ya mwezi wa Shabani, umeshuhudia usomwaji wa Dua Nnudba iliyohudhuriwa na kundi kubwa la zuwaru.

Dua imesomwa katika mazingira tulivu, kwa ushiriki wa zuwaru wa Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).

Atabatu Abbasiyya imeweka mazingira bora ya utekelezaji wa ibada hiyo, imeandaa vitabu vya dua, sehemu maalum ya kufanyia ibada na utoaji wa huduma za lazima kwa zuwaru.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: