Zuwaru wanasoma dua Nnudba katika haram ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s).

Ukumbi wa haram ya malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s), asubuhi ya Ijumaa ya kwanza katika mwezi wa Ramadhani, umeshuhudia usomaji wa dua Nnudba uliohudhuriwa na kundi kubwa la zuwaru.

Dua Nnudba imesomwa katika mazingira tulivu na kwa ushiriki wa kundi kubwa la zuwaru wa Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s).

Atabatu Abbasiyya huweka mazingira mazuri ya utekelezaji wa ibada hiyo, huandaa vitabu vya dua, sehemu maalum ya kufanyia ibada na hutoa huduma za lazima kwa mazuwaru.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: