Kiongozi wa idara hiyo bibi Adhraa Shami amesema: “Program imelenga kubainisha hukumu za kifiqhi kwa watumishi wa kike katika Ataba tukufu, chini ya utaratibu wa kukuza uelewa wa Dini”.
Akaongeza kuwa “Program inahusisha maelezo ya kina kuhusu hukumu za kifiqhi kwa wanawake, ili kuwafanya waelewe kwa usahihi hukumu za kisheria”.
Program hiyo ni sehemu ya harakati za kielimu zinazofanywa na idara, kwa lengo la kuimarisha elimu ya Dini kwa watumishi.



