Kwa picha.. makundi ya zuwaru yanahuisha usiku wa Ijumaa mbele ya Maqaam ya Imamu Mahadi (a.f)

Maqaam ya Imamu Mahadi (a.f) katika mji wa Karbala, imeshuhudia makundi ya zuwaru waliokuja kuhuisha usiku wa Ijumaa ya kwanza katika mwezi wa Dhulqaadah.

Wahudumu wa Maqaam wameweka mazingira mazuri kwa zuwaru wanaokuja kutoka ndani na nje ya Iraq.

Mji wa Karbala hupokea idadi kubwa ya watu wanaokuja kufanya ziara katika malalo ya Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) na kuhuisha utiifu wao kwa Ahlulbait (a.s).

Atabatu Abbasiyya imeandaa utaratibu kamili wa kutoa huduma bora kwa zuwaru na kukidhi mahitaji yao.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: