Kitengo cha Maqaam ya Imamu Mahadi (a.f) katika Atabatu Abbasiyya, kimeweka mabango yanayoashiria furaha kufuatia kumbukizi ya kuzaliwa Imamu Ridhwa (a.s).
Kazi hiyo imehusisha uwekaji wa mabango katika eneo linalozumguka Maqaam ya Imamu Mahadi (a.f) yaliyoandikwa maneno ya pongezi kufuatia kumbukizi ya tukio hilo tukufu.
Jambo hilo ni sehemu ya mkakati maalum wa kuadhimisha kumbukizi za mazazi ya Ahlulbait (a.s), kupitia kuweka muonekano unaoashiria furaha katika maeneo yanayozunguka Maqaam tukufu, jambo ambalo linasaidia kutengeneza mazingira bora ya kiimani kwa zuwaru.







