Watumishi wa kitengo cha kusimamia haram ya Atabatu Abbasiyya tukufu, wameweka mabango yanayoashiria furaha kufuatia kumbukizi ya kuzaliwa Imamu Ali bun Mussa Ridhwa (a.s).
Wameweka mapambo ya mabango kwenye korido zote za haram tukufu, yaliyoandikwa maneno ya pongezi kufuatia tukio hilo takatifu.
Jambo hilo ni sehemu ya mkakati wa kuhuisha kumbukizi za kuzaliwa Ahlulbait (a.s), kwa kuweka mapambo yanayoashiria furaha katika korido za haram tukufu.









