Baadhi ya ndugu wa mashahidi wa shule ya msingi Shajaratu-Twayyibah nchini Iran, wametembelea malalo ya Abulfadhil Abbasi (a.s).
Wamepokewa na kundi la wahudumu wa malalo takatifu, wageni wamefanya ibada ya ziara, dua, tenzi za husseiniyya zinazo omboleza vifo vya wanafunzi walio uwawa kwa kushambuliwa shule zao.
Wahudumu wa malalo takatifu wamewapa pole wafiwa na kuonyesha kuwa pamoja na familia za mashahidi, wamehimiza kupambika na subira na kuenzi kujitolea kwa mashahidi.






