Maahadi ya turathi za mitume (a.s) yatangaza kuanza kwa usajili wa awamu ya pili ya kuandaa wahubiri wa kike kwa masomo ya masafa..

Maoni katika picha
Baada ya mafanikio yaliyo patikana katika awamu ya kwanza ya kuandaa wahubiri wa kike kwa njia ya masafa, kwa kutumia mawasiliano ya kimtandao. Maahadi ya turathi za mitume (a.s) na masomo ya hauza kwa njia ya mtandao iliyo chini ya kitengo cha habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya tukufu imeamua kuanza usajili wa wanafunzi wa awamu ya pili kwa anuani isemayo (Kichuguu cha Zainabu kiadabu na kimaumbile), usajili umeanza tarehe mbili Rabiul Thani (1438 h) na utadumu kwa mwezi mmoja, masomo yataanza tarehe tano Jamadil Awwal (1438 h).

Zimesha andaliwa mada maalumu za kozi hii na kuwekwa katika mihadhara itakayo rushwa katika (YouTube) ya mtandao maalumu wa Maadadi, kila mshiriki ataweza kusikiliza mihadhara hiyo bure.

Mada zitakazo rushwa zitahusu masomo yafuatazo:

  • 1- Mada za Fiqhi.
  • 2- Mada za Akhlaq.
  • 3- Mada za Aqaaid.
  • 4- Maelezo ya historia za maimamu (a.s).
  • 5- Mihadhara kuhusu mimbari ya kihistoria na kimaudhui na namna ya uongeaji.

Kumbuka kua kozi hizi zinalenga kupunguza tatizo la wahubiri wa kike, na tunatarajia kupanua uga zaidi, hatimae kuboresha swala la majaalis (vikao) vya Husseiniyya vya kudumu, kwa namna na njia zinazo fahamika zaidi na zenye uhalisia na tukio. Pia idara ya mashindano katika Maahadi ya turathi za mitume (a.s) na masomo ya hauza kwa njia ya mtandao imeandaa zawadi ya mihadhara kumi ya mwanzo katika mashindano yatakayo fanyika mwishoni wa kozi.

Kwa maelezo zaidi au kushiriki katika kozi wasiliana nasi kwa: (07732907128).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: