Shule za Alkafeel za wasichana za tangaza kufanyika kwa kongamano la (Roho ya utume) na kufanyika kwa shindano la kitafiti kuhusu Zaharaa (a.s)..

Maoni katika picha
Idara ya shule za Alkafeel za wasichana iliyo chini ya kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinadamu katika Atabatu Abbasiyya tukufu imetangaza azma yake ya kufanya kongamano la (Roho ya utume) chini ya kauli mbiu isemayo: (Zahraa (a.s) ni hazina ya elimu na kilele cha hekima), na kufanya shindano la kitafiti la wanawake kuhusu bibi Fatuma Zaharaa (a.s) na wawaalika watafiti na wa andishi kushiriki katika shindano hilo. Shindano linalenga mambo yafuatayo:

Kwanza: Kubainisha athari ya fikra za kimalezi kuhusu Zaharaa (a.s) katika jamii ya kiislamu.

Pili: Kuangazia maswala ya kibinadamu katika kuitambua historia ya bibi wa wanawake duniani.

Tatu: Kupata somo na mazingatio kutokana na msimamo wake (a.s) katika kupigania haki za umma na maeneo matukufu.

Nne: kupata mazingatio kutokana na hoja zake kinaoshi katika kuthibitisha itikadi kwa njia ya mazungumzo.

Tano: Kuzipamba maktaba za kiislamu kwa tafiti bora za kielimu kutokana na historia yake (a.s).

Kutokana na tangazo, mada zitakazo shindaniwa zitakua ni:

  1. Athari za kiitikadi na kifiqhi kwa bibi Zaharaa (a.s).
  2. Uwanja wa kibinadamu na mfano mkuu wa mwenendo wa bibi Zaharaa (a.s).
  3. Msimamo wa bibi Zaharaa (a.s) katika kupigania haki na maeneo matukufu.
  4. Nyenzo za kutengenezea familia kutokana na mtazamo wa bibi Zaharaa (a.s).
  5. Mazungumzo ya bibi Zaharaa (a.s) kuhusu turathi za uislamu.

Mashariti ya mashindano ni:

  1. Utafiti wako usiwe umesha wahi kuchapishwa au kutolewa na watu wengine.
  2. Usiwe chini ya kurasa (12) na sio zaidi ya (20) ukubwa wa maandishi uwe saizi (16) kwa hati ya (matin) na saizi (14) kwa hati ya (simplified Arabic).
  3. Pamoja na nakala ya karatasi uwekwe na kwenye (CD) liandikwe jina la mtafiti (muandishi) pamoja na namba ya simu na wasifu (CV) yake. Yasipo zingatiwa hayo hautashugulikiwa.
  4. Aambatanishe na muhtasari wa utafiti wake usiozidi maneno (300).
  5. Mwisho wa kupokea tafiti hizo ni: (10 Jamadil Aakhir 1438h).
  6. Viandikwe vitabu rejea vyeto kwa namba za rejea katika karatasi ya mwisho.

Tafiti zitumwe katika anuani zifuatazo:

Idara ya shule za Alkafeel za kidini upande wa wasichana – kituo cha Swidiqatu Twahira (a.s) Karbala – mkabala na mtaa wa Usra- barabara ya hospitali ya Husseini.

Au kwa email: Fatema14asad@gmail.com

Unaweza kupiga simu: 07602345585 au 07732840851.

Zimesha andaliwa zawadi kwa washindi watatu wa mwanzo, ambazo ni:

  1. Mshindi wa kwanza milioni moja na laki tano (1,500,000) dinari za Iraq.
  2. Mshindi wa pili milioni moja na lakimbili na nusu (1,250,000) dinari za Iraq.
  3. Mshindi wa tatu milioni moja (1,000,000) dinari za Iraq.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: