Kituo cha turathi za Basra chahuisha wito wake kwa washiriki wa mashindano ya kwanza ya kimataifa ya kitabu kuhusu kuhusu Basra..

Maoni katika picha
Kituo cha turathi za Basra kilicho chini ya kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinadamu katika Atabatu Abbasiyya tukufu kimerejea wito wake kwa waandishi na watafiti wa kushiriki katika shindano la kimataifa la kwanza la uandishi wa kitabu kuhusu mji wa Basra, jambo hili litachangia kudhihirisha mema ya mji wa Basra na litatajirisha maktaba katika nyanja ya historia ya mji huo.

Shindano litahusisha mada zifuatazo:

  1. Maarifa ya Qur’an na tafsiri yake na mienendo za tafsiri pamoja na visomo vya Qur’an na mambo mengine yanayo husu Qur’an tukufu.
  2. Mada za kiakili na kiitikadi zitahusisha mambo tofauti ya kifikra, itikadi na falsafa za watu wa Basra.
  3. Mada za Fiqhi, Usulu, Diraya na hadithi.
  4. Mada za lugha, zitahusisha Nahau, Swarafu, Sauti, Balagha na mengineyo katika mambo yanayo husu maendeleo ya lugha na mchango wa watu wa Basra katika hilo.
  5. Mada za ushairi, zitahusisha aina tofauti za mashairi na mchango wa wanamashairi wa Basra ikiwa ni pamoja na mashairi ya Husseiniyya na Ahlulbait (a.s) kwa ujumla.
  6. Mada za kihistoria, zitahusisha historia ya mji wa Basra katika zama tofauti: kabla ya uislamu, wakati wa uislamu, zama za utawala wa Umawiyya, utawala wa Abbasiyya, tawala zingine, utawala wa Othmaniyya na hali ya zama hizi.
  7. Mada kuhusu maeneo matukufu na makaburi ya waja wema yaliyopo katika mji wa Basra (maelezo ya kina).
  8. Mada kuhusu elimu za watu wa Basra na mchango wao katika uwanja wa elimu tofauti.
  9. Historia kuhusu ujenzi wa mji wa Basra na mustakabali wake.
  10. Kuhakiki bitabu kale.
  11. Uhakiki yakinifu katika vitabu vilivyo andikwa kuhusu mji wa Basra katika nyanja tofauti.
  12. Mtazamo wa wanahabari kuhusu watu wa Basra.
  13. Siasa za watawala kuhusu watu wa Basra na athari ya siasa hizo katika ujenzi wa mji kifikra, kimajengo na kitamaduni na vinginevyo.
  14. Mada kuhusu athari na utalii.
  15. Mada kuhusu Jografia ya Basra ya zamani na ya sasa.
  16. Mada kuhusu uchumi wa Basra.

Zimeandaliwa zawadi kwa washindi kumi wa kwanza kama ifuatavyo:

  1. Zawadi ya kwanza: milioni tano dinari.
  2. Zawadi ya pili: milioni nne dinari.
  3. Zawadi ya tatu: milioni tatu dinari.
  4. Zawadi ya nne: milioni moja dinari.
  5. Zawadi ya tano: milioni moja dinari.
  6. Zawadi ya sita: milioni moja dinari.
  7. Zawadi ya saba: milioni moja dinari.
  8. Zawadi ya nane: milioni moja dinari.
  9. Zawadi ya tisa: milioni moja dinari.
  10. Zawadi ya kumi: milioni moja dinari.

Kutakua na zawadi zitakazo gawiwa kwa washiriki wengine pia, kumbuka kua mwisho wa kupokea tafiti (vitavu) vya washiriki ni (01/10/2017m) kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu katika namba zifuatazo: (07709050191 – 07604287317) au unaweza kuandika barua pepe kwa anuani ifuatayo: (basrah@alkafeel.net) au unaweza kutembelea ofisi zetu zilizopo: (Basra - barabara – Bagdad – mtaa Alghadeer – mkabala na mahakama kuu).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: