Hafla ya kuhitimisha mashindano ya kuhifadhi Qur’an tukufu yafanyika katika ukumbi wa haram ya Abbasi (a.s)..

Maoni katika picha
Katika ukumbi mtukufu wa haram ya Abulfadhil Abbasi (a.s) alasiri ya siku ya Juma Mosi (27 Jamadil Ula 1437h) sawa na (25/02/2017m) kimefanyika kikao cha mwisho cha mashindano ya kuhifadhi Qur’an tukufu yaliyo simamiwa na kituo cha kuandaa wasomi na mahafidh chini ya Maahadi ya Qur’an katika Atabatu Abbasiyya tukufu, washiriki walikua (60) kutoka katika matawi yote ya Maahadi ndani na nje ya Karbala, nayo ni miongoni mwa mradi wa kitaifa wa kuandaa mahafidh wa Qur’an tukufu.

Hafla ilifunguliwa kwa Qur’an tukufu uliyo somwa na Muhammad Muhsin Jauan mmoja wa wanafunzi wa Maahadi ya Qur’an tukufu, kisha ukafatia ujumbe wa uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu uliosomwa kwa niaba na mkuu wa Maahadi Shekh Jawadi Nasrawi, alianza kwa kutoa shukrani kwa kila aliye changia kufanikisha kwa mashindano haya, na akasema: “Hakika walio hifadhi Qur’an tukufu wana hadhi kubwa mbele ya Mwenyezi Mungu, imebainishwa na aya za Qur’an na kusisitiziwa na hadithi za maimamu wa Ahlulbait (a.s), mtu aliye hifadhi Qur’an anamalipo makubwa hulipwa pia mwalimu aliyemfundisha na kumsaidia aweze kuhifadhi Qur’an na wazazi wake walio mshajihisha, mashindano haya ni kwa ajili ya kujenga moyo wa kuongeza juhudi katika kuhifadhi, yamefanikiwa katika mpangilio wake na ushiriki pia siku za mbele mtashuhudia mashindano kama haya ya walio hifadhi Qur’an nzima”.

Akaongeza kua: “Hakuna aliye feli katika mashindano haya, wote mmefaulu mmepata malipo makubwa na mtaendelea kushiriki katika mashindano ya kitaifa na kimataifa”.

Baada ya hapo yalifanyika maonyesho ya kuhifadhi Qur’an tukufu na wanafunzi walioshiriki katika mashindano, alianza Mustafa Saaduni ambaye amehifadhi juzuu ishirini, kwa kuulizwa maswali na wahudhuriaji, walimuuliza aya ya kwanza katika sura na yeye akawa anasoma aya zinazo fuata hadi mwisho, kisha akafuata Ali Raadi Muhammad aliye hifadhi juzuu tatu, pia aliulizwa na wahudhuriaji kwa kusomewa aya na yeye anataja namba ya aya hiyo, sura na ukurasa kisha anaisoma na anaendelea kusoma aya zinazo fuata.

Halafu kulikua na ujumbe wa majaji uliosomwa kwa niaba na jaji wa Qur’an Ustadh Qassim Hami, alisema kua: “Hakika mashindano haya ni sawa na mashindano ya kitaifa, kutokana na namna yalivyo endeshwa, hii ni kutokana na juhudi zilizo fanywa na Maahadi pamoja na kituo cha kuandaa wasomi, kimeweza kutuletea mahafidhi bora watakao wakilisha Iraq katika mashindano ya kimataifa, shukrani za dhati ziwaendee washiriki na walimu wao, kamati ya majaji imetumia utaratibu unao tumika hapa Iraq na nje ya Iraq, na Maahadi iliweka masharti mazuri sana yamewasaidia mahafidh kuendeleza vipawa vyao na kusoma kwa kufuata hukumu, hakika zoezi lilikua zuri na litakua na mustakbali mzuri”.

Kisha kamati ya majaji walitangaza majina ya walioshinda na kuwapa zawadi, washindi walikua kama wafuatavyo:

Walio hifadhi juzuu moja:

  • 1- Amiri Ahmadi Aajil
  • 2- Mustafa Muhammad Jafari
  • 3- Ali Karari Swalehe

Walio hifadhi juzuu tatu:

  • 1- Muhammad Hussaam Muhsin
  • 2- Mussa Faiz Qassim
  • 3- Ali Raadu Muhammad

Walio hifadhi juzuu tano:

  • 1- Ibrahim Maitham Muhammad
  • 2- Wasam Khawaam Abdulkadhim
  • 3- Muqtada Mushtaqu

Walio hifadhi juzuu kumi:

  • 1- Sajadi Hussein
  • 2- Abbasi Haidari Muhammad
  • 3- Murtadha Raid Awadi

Walio hifadhi juzuu kumi na tano:

  • 1- Haidari Falihu Rashidi
  • 2- Hussein Anisi Muhsin
  • 3- Halikutajwa jina lake kwa kutopata max zilizo takiwa

Walio hifadhi juzuu ishirini:

  • 1- Hassan Muhammad Jaasim
  • 2- Muhammad Alawi Hassan
  • 3- Mustafa Saaduni Jaabir
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: