Ndege zisizo na rubani za kikosi cha Abbasi (a.s) cha wapiganaji zashambulia magaidi ya daesh upande wa kulia wa mji wa Mosul..

Maoni katika picha
Baada ya mafanikio makubwa yaliyo patikana kwa wapiganaji wa aridhini wa kikosi cha Abbasi (a.s) yaliyo pelekea kukombolewa maeneo makubwa yaliyo kua chini ya udhibiti wa magaidi ya daesh, kuna maendeleo mengine muhimu yamepatikana katika vikosi vya anga, ndege za kivita zisizo kua na rubani zimefanya shambulizi kubwa dhidi ya magaidi ya daesh.

Shambulizi hilo limetokana na taarifa za kina zilizo patikana kutokana na ndege za upelelezi za kikosi hiki cha Abbasi (a.s), baada ya kunasa harakati za adui magaidi ya daesh tuliwasambaratisha kwa kuwashabulia na kuwapa hasara kubwa ya watu na mali, na ndege zote zilirudi salama katika vituo vyake.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: