Kukamilika kwa maandalizi ya kongamano la kimataifa kuhusu uhuishaji wa mimbari ya Husseiniyya..

Maoni katika picha
Kamati ya maandalizi ya kongamano la kimataifa la kuhuisha mimbari ya Husseiniyya litakalo fanywa na Atabatu Abbasiyya kwa kushirikiana na taasisi ya Bahrul Ulumi Alkhairiyya, imetangaza kukamilika kwa maandalizi yote na kongamano litaanza siku ya Alkhamisi (17 Jamadil Aakhira 1438 h) sawa na (16 Machi 2017 m) katika ukumbi wa taasisi ya Bahrul Ulumi ndani ya mji wa Najafu, chini ya kauli mbiu isemayo: (Hauza za kielimu ni msingi wa uhuishaji), kongamano litakua na anuani isemayo (Kongamano la kimataifa kuhusu uhuishaji wa mimbari ya Husseiniyya) na litafanyika siku mbili, taarifa ikafafanua kua: “Siku ya kwanza kutakua na hafla ya ufunguzi, ambayo ni siku ya Alkhamisi (16 Machi 2017 m) sawa na (17 Jamadil Aakhira 1438 m) katika mji wa Najafu ndani ya ukumbi wa jengo la taasisi ya Bahrul Ulumi Alkhairiyya, na kutakua na mada zidakazo tolewa asubuhi na jioni, siku ya pili ya kongamano, ambayo itakua siku ya Ijumaa (17 Machi 2017 m) sawa na (18 Jamadil Aakhira 1438 h) vikao vitafanyika katika Atabatu Abbasiyya na mada zitatolewa asubuhi na jioni pia kutakua na hafla ya ufungaji wa kongamano”.

Kamati ya maandalizi ikaendelea kusema kua: “Kuna kamati ya wataalamu imeundwa na wanachuoni wa hauza na wasomi wa kisekula, watakao chuja mada zitakazo wasilishwa katika viwango vya kielimu kwa kufuata kanuni zinazo tambulika, ili kongamano liendane na malengo yake na uwe msingi imara wa muendelezo wa makongamano mengine yenye manufaa zaidi katika hauza ya Najafu, mialiko ilitolewa kwa wasomi wa hauza na wa kisekula ili waweze kushiriki, mada zitakazo tolewa ni:

Sehemu ya kwanza: Makhatibu wa Husseiniyya

  1. Maendeleo ya kihistoria katika mimbari ya Husseiniyya.
  2. Vigezo vya kielimu kwa khatibu (mzungumzaji).
  3. Changamito za sasa zinazo shambulia mimbari ya Husseiniyya.
  4. Vitisho vya kielimu katika mada zinazo wasilishwa.
  5. Sifa za pekee katika hotuba za Husseiniyya.
  6. Umuhimu wa mimbari za Husseiniyya katika jamii na dini.
  7. Athari zilizopo katika kuainisha madhumuni ya hotuba.
  8. Nafasi ya mimbari ya Husseiniyya katika kudumisha uislamu.
  9. Mimbari ya Husseiniyya kati ya uasili na uhuishwaji wake.

Sehemu ya pili: Utajiri wa swala la Husseiniyya

  1. Nafasi ya utajiri wa swala la Husseiniyya.
  2. Nafasi ya utajiri katika kusisitizia upande wa kimaumbile.
  3. Kutofautiana malengo ya utajiri kutokana na kutofautiana kwa hali za jamii.
  4. Adabu katika swala la Husseiniyya.
  5. Maendeleo yake katika hisia za watu.
  6. Visa na matukio vinapingana au vinaoana.

Sehemu ya tatu: Makhatibu na washairi katika swala la Hussein.

  1. Shekh Muhammad Ali Ya’aqubiy
  2. Sayyid Swaleh Hilliy
  3. Sayyid Jawaad Shibri
  4. Shekh Ahmad Waailiy
  5. Sayyid Ridha Hindiy
  6. Shekh Abdul-muni’imu Fartusi

Kumbuka kua kongamano hili, lina umuhimu mkubwa wa kusambaza tamaduni za Ahlulbait (a.s) na kueneza maana ya uislamu mtukufu katika jamii inayo kubwa na vikwazo kutoka kila upande, kifikra, kiteknelojia, katika mitandao ya kijamii, na uharaka wa kusafirisha habari uliopo hivi sasa bila vikwazo vyovyote.. jambo ambalo limeonyesha umuhimu mkubwa kwa wazungumzaji wa mimbari ya Husseiniyya wenye aina zote za utukufu, uadilifu na roho ya kuvumiliana, na kuachana na kila aina ya ubaguzi na chuki zinazo pelekea uhasama, kupigana na kutengana baina wa waislamu, wazungumzaji wa mimbari ya Husseiniyya waenzi utamaduni wao wa kuhakikisha waislamu wanaishi kwa amani na watu wote.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: