Kamati ya maandalizi ya kongamano la pili kuhusu fatwa tukufu ya kujilinda yatangaza mashindano ya filamu za mfano kuhusu Hashdi Sha’abi na yawataka wataalamu wa filamu wajitokeze..

Maoni katika picha
Kamati ya maandalizi ya kongamano la pili kuhusu fatwa tukufu ya kujilinda yawaomba wataalamu wa filamu wajitokeze katika mashindano la filamu ya mfano itakayo onyesha ushujaa na ujasiri wa jeshi la Iraq na wapiganaji wa Hashdi Sha’abi yatakayo fanyika katika kongamano hilo, litakalo simamiwa na kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu, kama sehemu ya kumbukumbu ya kutolewa kwa fatwa tukufu ya kujilinda, chini ya kauli mbiu isemayo (Fatwa..ni chemchem ya ushindi na miski ya shahada).

Kamati imeweka kanuni na taratibu zifuatazo:-

  • 1- Fikra ya filamu iendane na mtazamo wa kongamano.
  • 2- Filamu ionyeshe ushujaa na ujasiri wa jeshi la Iraq na Hashdi Sha’abi kwa ujumla (sio kumlenga mtu) katika kulinda nchi, misingi ya kibinadamu, mazingira na maeneo matukufu.
  • 3- Filamu isiwe imesha wahi kuonyeshwa katika vyombo vya habari au mitandao ya kijamii au katika maonyesho mengine.
  • 4- Filamu itakayo shiriki ihifadhiwe katika CD na iwasilishwe katika kitengo cha Habari na Utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu, ikiambatana na wasifu (CV) ya muandaaji, au tuma katika email ifuatayo (info@holyfatwa.com).
  • 5- Mwisho wa kupokea filamu hizo ni 05/05/2017 m.
  • 6- Filamu isiwe chini ya dakika moja na zisizidi dakika ishirini (20).
  • 7- Aina ya filamu iwe (HD au avi).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: