Kamati ya maandalizi ya kongamano la kitamaduni la fatwa tukufu ya kujilinda yawaomba watafiti na waandishi washiriki katika shindano la kitafiti na kitamaduni walilo andaa..

Maoni katika picha
Kamati ya maandalizi ya kongamano la fatwa tukufu ya kujilinda yawataka waandishi na watafiti washiriki kwenye shindano litakalo fanyika katika kongamano litakalo simamiwa na kitengo cha habari na utamaduni cha atabatu Abbasiyya tukufu, la kumbukumbu ya kutolewa kwa fatwa ya kujilinda chini ya kauli mbiu: (Fatwa.. ni msingi wa ushindi na miski ya shahada).

Wametaja mada zitakazo shindaniwa kuwa ni:-

Kwanza: Nafasi ya vyombo vya habari katika kuhuisha na kudumisha uzalendo kabla ya ukombozi na maada yake.

Pili: Mapambano ya vyombo vya habari dhidi ya taasisi za kitaifa na kimataifa zinazo unga mkono ugaidi pamoja na vyombo vya habari vya madaesh na wafuasi wao.

Tatu: Nafasi chanya ya vyombo vya habari kwa Ataba katika kufikisha fatwa tukufu kwa jamii ya kitaifa na kimataifa na kujibu upotoshaji na uzushi kuhusu swala hilo.

Nne: Kufanyiwa kazi usia na maelekezo ya Marjaa kwa wapiganaji ndani ya uwanja wa vita.

Tano: Matendo ya kibinadamu na kizalendo yanayo fanywa na wapiganaji katika vita ya ukombozi.

Sita: Athari chanya ya jamii na familia za wairaq katika kuwaandaa watu wake kukubali fatwa na kujitolea kwa ajili ya kukomboa nchi yao.

Saba: Undani wa kihistoria wa fatwa tukufu ya kujilinda, na athari yake katika kuamsha moyo wa Husseiniyya.

Nane: Juhudi za watu wa sekula katika kuthibitisha na kufundisha mambo yanayo tokea.

Tisa: Nafasi ya mitandao ya kijamii na athari yake katika kubainisha ubinadamu na uzalendo na kuwajibu waovu na wapotoshaji wa habari.

Sharti za ushiriki ni hizi zifuatazo:

  • 1- Makala isiwe chini ya kurasa (20) na zisizidi (25).
  • 2- Makala iandikwe kwa hati ya (simplified Arabic) ukubwa wa herufi uwe saizi (16).
  • 3- Utafiti uendane na malengo ya kongamano na uwe ndani ya mada tajwa hapo juu.
  • 4- Mwisho wa kupokea Makala zitakazo shindanishwa ni (05/05/2017 m).
  • 5- Makala iandikwe na kuhifadhiwa katika (CD) Na iwasilishwe katika ofisi za kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu au itumwe katika barua pepe ifuatayo, (info@holyfatwa.com).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: