Usiku na mchana wa Mab’ath tukufu ya mtume, ubora na a’amali zake..

Maoni katika picha
Imepokewa kutoka kwa Abuu Jafari Jawaad (a.s) anasema: (Hakika katika mwezi wa Rajabu kuna usiku bora kuliko kila kitu kinacho angaziwa na jua, nao ni usiku wa mwezi ishirini na saba, asubuhi ya usiku huo alipewa utume (s.a.w.w), mtu mwenye kufanya ibada siku hiyo anaandikiwa thawabu za ibada ya miaka miwili), siku hiyo ni miongoni mwa siku muhimu zaidi, nayo ni miongoni mwa sikukuu tukufu, katika siku hiyo Jibril (a.s) alishuka na ujume wa utume wa Muhammad (s.a.w.w).

Kuna ibada na dua maalumu katika usiku wa Mab’ath miongoni mwake ni:

  • 1-
  • 2- Swala ya rakaa kumi na mbili iliyo pokewa kutoka kwa imamu Muhammad bun Ali Jawaad (a.s).
  • 3- Ziara ya Amirulmu-uminina Ali bun Abuutwalib (a.s).
  • 4- Kusoma dua ya “Allahumma inni as-aluka bitajallil a’adhami fi hadhihi llailat mina shahril adhim..”.

Siku ya ishirini na saba Rajabu alipewa rasmi ujumbe wa uslamu mtukufu (s.a.w.w) miaka (13) kabla ya kuhama Maka na kwenda Madina, ulikua ni mwaka wa (610 m), Mwenyezi Mungu alimletea wahyi kupitia Jibril na kumjulisha rasmi kua yeye ni mtume wa umma huu na ndiye mtume wa mwisho..

Miongoni mwa ibada muhimu katika siku hii ni:

  • 1-
  • 2- Kufunga, atakae funga siku hii itakua kafara kwake kwa mwezi sitini.
  • 3- Kukithirisha kumswalia mtume Muhammad na Aali zake watakatifu.
  • 4- Ziara ya khatamul anbiyaa wa sayyidul mursalina Muhammad (s.a.w.w) na ziara ya Amirulmu-uminina Ali bun Abuutwalib (a.s).
  • 5- Kuswali rakaa thelathini, katika kila rakaa baada ya surat Fat-ha usemo surat Tauheed mara kumi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: