Kwanza: Mada za kifikra na kiitikadi.
- 1- Nafasi ya mwanamke katika kujenga jamii yenye itikadi sahihi na fikra za muhanga wa imamu Hussein (a.s).
- 2- Tukio la Karbala na athari chanya katika kukuza hisia za mwanamke kuhusu kudhulumiwa na kutenzwa nguvu.
- 3- Nafasi ya mwanamke katika kuonyesha mateso na dhulma za tukio la Twafu.
- 4- Upambanaji wa mwanamke kihistoria katika kuhuisha misingi ya muhanga wa imamu Hussein (a.s).
- 5- Ukubwa wa imani katika maneno ya wanawake katika msafara wa imamu Hussein (a.s).
- 6- Nafasi ya mwanamke kifikra katika kueneza misingi ya muhanga wa imamu Hussein (a.s) na malengo yake.
Pili: Mada za ki-akhlaqi na kijamii.
- 1- Mwanamke Zainabiyya baina ya kujichunga na kutekeleza wajibu wake katika jamii.
- 2- Matokeo chanya ya uwepo wa bi Zainabu katika msafara wa Imamu Hussein (a.s) na athari yake kwa watumishi na mazuwaru.
- 3- Mtumushi wa kike! Mubalighah na nafasi yake katika kutangaza mafunzo ya dini kwa mazuwaru.
- 4- Mtazamo wa jamii kidini kuhusu uwepo wa wanawake katika malalo matukufu na katika misimu ya mazuwaru wengi (mamilioni).
- 5- Mtazamo wa kijamii katika kugawa majukumu baina ya wanaume na wanawake (msafara wa imamu Hussein) kama mfano.
Tatu: Mada za kilugha
- 1- Utungaji wa mashairi kuhusu imamu Hussein (a.s) na uimbaji katikati ya wanawake.
- 2- Nafasi ya fani za lugha kwa mwanamke katika kutangaza swala la imamu Hussein (a.s) na kulirithisha kwa vizazi vijavyo.
- 3- Washairi kuathiriwa na mwanamke na nafasi yake katika tukio la Karbala.
- 4- Ufaswaha wa mwanamke katika swala la imamu Hussein (a.s) na athari yake kwa wapokeaji.
Fahamu kua mwisho wa kupokea tafiti hizo ni Juma Tano ya tarehe 20/09/2017m, washiriki watafahamishwa kuhusu kukubaliwa ushiriki wao tarehe 15/10/2017m.
Tafiti hizo ziwasilishwe katika taasisi ya Waarithul-Anbiyaau chini ya Atabatu Husseiniyya tukufu katika ofisi zake zilizopo Najafu Ashrafu mtaa wa Hannaana, au kupitia anuani yake ya barua pepe: almarafikarbala@warithanbia.com pia unaweza kupiga simu: (07708730666 – 07813053831) au unaweza kuwasilisha katika Atabatu Abbasiyya idara ya wanawake kupitia barua pepe: library@alkafeel.net au piga simu namba: (07716199086 – 07826143083).
Kiongozi wa idara ya wanawake katika kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu ameuambia mtandao wa kimataifa Alkafeel kua; kongamano hili miongoni mwa mambo muhimu linalo lenga ni:
- 1- Kuchangia katika kuonyesha nafasi ya mwanamke kielimu na athari yake katika kufanikisha muhanga wa imamu Huseein (a.s) na malengo yake.
- 2- Kuinua kiwango cha kutafakari cha watumishi wa kike katika Ataba na mazaru tukufu.
- 3- Kudhihirisha uwezo wa kifikira na kitamaduni alio nao mwanamke na kusimamia itikadi yake katika misingi anayo iamini.
- 4- Kuonyesha nafasi ya mwanamke katika kurekebisha jamii na mtu mmoja mmoja.
- 5- Kubadilishana fikra na kuunganisha juhudi za wanawake wanao fanya kazi katika Ataba na Mazaru za kidini tukufu.
- 6- Kusimama dhidi ya watu wanao shambulia na kujaribu kuharibu picha halisi ya mwanamke na kuzusha shubha katika dini tukufu ya kiislamu.