Maelfu ya waumini kutoka ndani na nje ya Iraq wamefurika katika uwanja wa katikati ya haram mbili tukufu (Husseiniyya na Abbasiyya) wakifanya ibada na kusoma dua za siku ya Arafa jirani na imamu Hussein (a.s) katika siku hii muhimu, aliye pata utukufu wa kuendesha program hiyo ni Shekh Maitham Tamaar.
Watumishi wa eneo ya katikati ya haram mbili wameweka mazingira vizuri kuhakikisha watu wanafanya ibada kwa urahisi na utulivu.
Kumbuka kua viwanja vya haram mbili ya imamu Hussein na Abulfadhil Abbasi (a.s) vimejaa mazuwaru, ndani ya viwanja hivyo pia kumefanyika program ya usomaji wa dua za Arafa.