Kuanzishwa kwa sehemu mpya za kuhifadhia mabeji na vifaa vya mazuwaru katika ziara ya Arubaini..

Maoni katika picha
Kutokana na jukumu walilonalo idara ya Amanaat iliyo chini ya kitengo cha utumishi katika Atabatu Abbasiyya tukufu, wamefungua sehemu mpya za kuhidhia vitu vya mazuwaru wanaokuja katika Ataba tukufu za Karbala kufanya ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s), fahamu kua mabeji yanahitaji sehemu pana, kama yasipo hifadhiwa katika vibanda vya Amanaat vilivyo zunguka haram tukufu ya Abulfadhil Abbasi (a.s) ambako hua kuna msongamano mkubwa sana wa watu. Ndio tukaamua kutengeneza sehemu hizi kwa ajili ya kupunguza msongamano wa watu katika vibanda vya zamani.

Kwa mujibu wa maelezo ya kiongozi wa idara hiyo, Ustadh Muhammad Habibu Jibri, amesema kua: “Tumefanya hivi kutokana na malengo tuliyo jiwekea ya kuhakikisha tunafanya kila linalo hitajiwa na watu wanaokuja kufanya ziara kutoka ndani na nje ya nchi, ambao idadi yao inaongezeka kila siku kadri msimu wa ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s) inavyo karibia, tumeandaa sehemu tatu zilizo chaguliwa kutokana na sehemu hizo kua na msongamano mkubwa wa watu, nazo ni:

  • 1- Katika eneo la mlango wa Kibla wa Abulfadhil Abbasi (a.s) eneo linaukubwa wa mita (3000).
  • 2- Katika eneo la uwanja wa Juud, eneo lenye ukubwa wa mita (200).
  • 3- Katika eneo la mlango wa Bagdad (Baabu Bagdad), eneo lenye ukubwa wa mita (250).

Akabainisha kua: “Maeneo haya ni makubwa, yanauwezo wa kuhifadhi maelfu ya mabeji, zimetengenezwa shelfu (kabati) zinazo endana na ukubwa wa kila eneo, tayali wamesha pangwa watumishi watakao kaa sehemu hizo muda wote, kila mtu atakaye hifadhi beji lake hapo atapewa namba maalum atakayo takiwa kuonyesha wakati wa kuchukua beji lake”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: