Kwa kushirikiana na Ataba mbili tukufu Husseiniyya na Abbasiyya, taasisi ya Qabsu Lithaqaafah wa Tanmiyya, yajiandaa kufanya kongamano la kwanza la kitamaduni..

Maoni katika picha
Kufuatia ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s) na juhudi kubwa zinazo fanywa na taasisi mbalimbali kwa ajili ya kunufaika na mazingira ya ziara hii, manufaa yanayo endana na malengo ya harakati ya Imamu Hussein (a.s), taasisi ya Qabsu Lithaqaafah wa Tanmiyya kwa kushirikiana na Ataba mbili tukufu, Husseiniyya na Abbasiyya wanajiandaa kufanya kongamano la kwanza.

Msimamizi mkuu wa jambo hilo Shekh Twariq Bagdady amebainisha kua: “Hakika ziara ya Arubaini ya mwaka huu, itashuhudia kufanyika kwa kongamano la kwanza la (Msimu wa kitamaduni) chini ya usimamizi wa taasisi ya Qabsu Lithaqaafah wa Tanmiyya ikishirikiana na Ataba mbili tukufu (Husseiniyya na Abbasiyya) na kushiriki jopo la wasomi kutoka katika vyuo vikuu vya Iraq”.

Akafafanua kua: “Hakika huu ni mradi wa kwanza wa aina hii, unalenga kunufaika na mazingira ya kiroho yanayo patikana kwa mazuwaru, kwa ajili ya kutatua matatizo ya kijamii, kitamaduni, kimalezi na kifikra kupitia vituo vitakavyo funguliwa na mradi huu, ambavyo ni:

  • - Kituo cha kulinda familia.
  • - Kituo cha kutakasa tamaduni na tabia.
  • - Kituo cha kusimamia vijana.
  • - Kituo cha fani na adabu.
  • - Kituo cha habari na athari zake katika jamii.

Shekh Bagdady akaongeza kusema kua: “Tunatarajia kua na matokeo mazuri katika kongamano hili, na kuweka msingi utakao tuwezesha kuifikia mikoa yote na kuunda kamati mbalimbali za vijana wenye uweledi na moyo wa kujitolea, watakao kufanya kazi katika sekta mbalimbali na miji tofauti baada ya msimu wa ziara”
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: