Idara ya uhusiano ya Atabatu Abbasiyya tukufu yawashirikisha zaidi ya wanafunzi wa vyuo 400 katika kutoa huduma kwa mazuwaru wa Arubaini…

Maoni katika picha
Idara ya uhusiano wa vyuo vikuu chini ya kitengo cha mahusiano katika Atabatu Abbasiyya tukufu, imeshirikisha zaidi ya wanafunzi wa vyuo vikuu 400 katika kazi mbalimbali za kutoa huduma zilizo pangwa na Ataba tukufu, hii sio mara ya kwanza kuwashirikisha wanafunzi na watu wengine katika utoaji wa huduma, wamesha shirikishwa mara nyingi, na kuna baadhi ya idara zinahitajia zaidi msaada ya wanafunzi hawa.

Kwa mujibu wa maelezo ya kiongozi wa idara ya mahusiano Ustadh Azhar Rikaabiy, amesema: “Wanafunzi hawa kabla ya muda mfupi tulifanya makubaliano nao kwa kutumia wawakilishi wetu waliopo katika vyuo vikuu vya Iraq, tukawaomba washiriki katika utoaji wa huduma kwenye ziara ya Arubaini, na tulifanya nao vikao mbalimbali na kuwaelezea kazi watakazo fanya katika siku za ziara, kupitia vikao vivyo tuliwagawa kutokana na uhitaji wa vitengo vya Ataba, tuliwagawa katika maeneo yafuatayo:

  • 1- Vituo vya wapotelewa.
  • 2- Vituo vya uelekezaji.
  • 3- Vituo vya afya.
  • 4- Vituo vya upimaji wa afya.
  • 5- Vituo vya huduma ya kwanza na magari ya wagonjwa.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: