Kwa ajili ya kuendana na ulimwengu wa habari wa kisasa na kufuatilia matukio yanayo gusa jamii ya kiislamu, jarida ya (Rasdi) latoka kwa sura mpya na kuzingatia mada muhimu…

Maoni katika picha
Baada ya kupita miaka miwili tangu kuanzishwa kwake, jarida la (Rasdi) linalo tolewa na kituo cha kiislamu cha masomo ya kimkakati chini ya kitengo cha habari na utamaduni katika Atabatu Abbasiyya tukufu, sasa linatoka katika muonekano mpya likiwa limesheheni matukio mbalimbali, ya kisiasa, kiuchumi, kijeshi na kitamaduni yenye uhusiano mkubwa na ulimwengu wa kiislamu pamoja na wafuasi wa Ahlulbait (a.s).

Utaratibu wa jarida la Rasdi unao fatwa na kituo cha kiislamu ni ule wa kunukuu tukio kama lilivyo tokea bila kuongeza wala kupunguza pamoja na kuangalia namna vyombo vya habari vilivyo ripoti tukio hilo, na kisha kuangalia kilicho nyuma ya pazia, kazi hiyo inafanywa na waandishi mahiri walio bobea, kisha wanakuja na msimamo wa kati bila kuegemea upande wowote,

Jarida hili lina waandishi nguli (walio bobea) katika sekta ya habari, na wamejikita katika mada kuu nne, ambazo ni:

  • 1- Mada zinazo husu ulimwengu wa kiislamu.
  • 2- Mada zinazo husu mchanganyiko wa tamaduni.
  • 3- Mada zinazo husu Ushia na Mashia.
  • 4- Mambo yanayo husu mambo ya Iraq.

Fahamu kua jarida hili halisambazwi sana, nalo linalenga kutoa mtazamo sahihi kwa watu wenye mamlaka na vyombo vya maamuzi, unapo tokea utata katika jambo lenye athari kwa jamii.

Ukitaka kuangalia zaiti kuhusu uandaaji wa jarida hili ingia hapa: http://www.iicss.iq/?id=38
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: