Wanafunzi wa shule za Ameed wanashiriki katika ratiba za msimu wa huzuni wa kumi zinazo fanywa kuhuisha kifo cha Zaharaa (a.s)…

Maoni katika picha
Katika kuhuisha kumbukumbu ya kifo cha mbora wa wanawake wa ulimwenguni Swidiqah Fatuma Zaharaa (a.s), wanafunzi wa shule za Ameed wameshiriki katika ratiba inayo endeshwa pembezoni mwa program za msimu wa huzuni wa kumi unao simamiwa na kitengo cha mawakibu na maadhimisho ya Husseiniyya chini ya Ataba mbili tukufu katika eneo la katikati ya haram mbili tukufu.

Ratiba hiyo inatekelezwa kwa ajili ya kujenga uwelewa wa msimu wa huzuni za Fatwimiyya kwa wanafunzi wa shule za Ameed, ambapo wanafunzi walio shiriki wametoka katika shule za (Shule ya msingi ya wasichana Al-Ameed, Shule ya msingi ya wavulana Al-Ameed, Shule ya msingi ya wasichana Al-Qamaru, Shule ya msingi ya wavulana Saaqi, Shule ya msingi ya wavulana Sayyidul-Maa na Shule ya msingi ya wavulana Nurul-Ameed).

Katika program ya uchoraji wameshiriki zaidi ya wanafunzi thelathini na tano wavulana na wasichana kutoka katika shule za Ameed, kama sehemu ya kukumbuka dhulma alizo fanyiwa bibi Fatuma Zaharaa (a.s) ambapo wamechora moja kwa moja (live) katika karatasi.

Katika msimu huu wa huzuni za Fatwimiyya unao simamiwa na kitengo cha mawakibu na maadhimisho ya Husseiniyya chini ya Ataba mbili tukufu kwa muda wa siku kumi kunahusisha vitu vingi, ikiwa ni pamoja na (Panorama) kutengeneza sauti na picha za riwaya zinazo elezea kisa cha kudhulumiwa kwake (a.s) na tamasha la uchoraji kwa watoto walio chini ya miaka kumi pamoja na majlisi za kuomboleza na vitu vingine.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: