Kufuatia pongezi za washiriki: Kitengo cha habari na utamaduni chakalilisha ratiba ya wanafunzi wa chuo cha Alkafeel…

Maoni katika picha
Wanafunzi wa chuo kikuu cha Alkafeel wamesifu ratiba waliyo pangiwa na kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu katika kipindi hiki cha likizo, wamethibitisha kua wamenufaika sana kutokana na ratiba hiyo, wakatoa shukrani pia kwa wasimamizi wa ratiba hiyo, walio fanya kazi kubwa kuhakikisha wanaitekeleza, na kufikia malengo tarajiwa, wakatoa wito wa kurudiwa jambo hili siku za mbele.

Ratiba yenyewe ni hema la kitamaduni lililo kua na mambo mbalimbali yanayo endana na kiwango cha elimu na umri wa washiriki, chini ya usimamizi wa kamati ya watalam walio bobea, na kulikua na mihadhara elekezi ya kidini na kuhusu maendeleo ya kibinadamu, pamoja na vipindi vya mapumziko na kutembelea Ataba tukufu na miradi ya Atabatu Abbasiyya ya kiviwanda na kielimu.

Wakati wa kufunga ratiba ya hema washiriki wote walipewa vyeti vya ushiriki, na wale walio fanya vizuri katika mashindano wakapewa zawadi.

Fahamu kua ratiba hii iliandaliwa kwa ajili ya kunufaika na kipindi cha likizo na kuongeza elimu na maarifa pamoja na kulea vipaji na kuwafanya waweze kutumia vipawa vyao katika maisha ya nyumbani na chuo, hali kadhalika kuwaweka karibu na malalo ya maimamu wao, ambayo ni moja ya vituo muhimu kielimu na kiutamaduni kutokana na harakati mablimbali zinazo fanywa na malalo hizo tena katika sekta tofauti.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: