Mwaliko wa kushiriki shindano la kitaifa kuhusu uandishi wa visa vya watoto kufuatia ujasiri wa wanajeshi wetu na Hashdi Sha’abi…

Maoni katika picha
Uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu unatoa mwito kwa watalamu wa tamaduni na adabu za watoto waje kushiriki katika shindano la kitaifa, litakalo husu uandishi wa visa vya watoto kuhusu ujasiri wa wanajeshi wetu na Hashdi Sha’abi, pamoja na visa vya kujitolea na vinavyo ashiria uzalendo wa taifa, Shindano hilo litafanyika sambamba na kongamano litakalo endeshwa na kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu linalo adhimishwa kwa mara ya tatu tangu kutolewa kwa fatwa tukufu ya kujilinda, chini ya kauli mbiu isemayo (Ushindi umetokana na nyie ni wenu na nyie ndio wenye nao).

Kamati inayo simamia shindano hili imeweka masharti yafuatayo:

  • A- Kisa kiandikwe kwa kufuata misingi ya kiutalamu na maadili ya watoto.
  • B- Kielezee ujasiri wa jeshi la Iraq na Hashdi Sha’abi kwa ujumla (sio kumuelezea mtu maalum) katika kulinda taifa na misingi ya ubinadamu na jinsi walivyo linda mazingira na maeneo matakatifu.
  • C- Kisa kisiwe kimesha wahi kuandikwa katika kitabu au mitandaoni au kimesha wahi kutolewa katika shindano lingine.
  • D- Kiandikwe kwa kutumia program ya (ward) na kihifadhiwe kwene (CD) kisha kikabidhiwe kwenye kitengo cha habari na utamaduni cha Atabatu Abbasiyya tukufu, kikiwa pamoja na wasifu (cv) ya muandishi, au kinaweza kutumwa kwenye mtandao wa kimataifa Alkafeel ambao ni (alkafeel.net) au kwenye anuani ifuatayo (info@holyfatwa.com).
  • E- Mwisho wa kupakea ni tarehe 21 Juni 2018m.
  • F- Zimeandaliwa zawadi kwa visa vitano vitakavyo faulu ambazo ni (200,000) dinari laki mbili za Iraq.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: