Maktaba na Daru Makhtutwaat ya Atabatu Abbasiyya tukufu yahitimisha nadwa ya kielimu kuhusu nafasi ya maktaba katika mpango wa maendeleo endelevu hadi mwaka (2030)…

Maoni katika picha
Ukumbi wa Imamu Hassan (a.s) katika Atabatu Abbasiyya tukufu asubuhi ya Ijumaa (29 Jamadal-Awwal 1439h) sawa na (16 Februari 2018m) ulikua mwenyezi wa kikao cha kufunga nadwa iliyo andaliwa na kusimamiwa na kituo cha faharasi na kupangilia maalumaat kilicho chini ya maktaba na daru makhtutwaat ya Ataba tukufu, iliyo hudhuriwa na watafiti wabobezi kutoka ndani na nje ya Iraq.

Mijadala ya nadwa ya siku ya pili ilisimamiwa na Dokta Jasim Jarjis kutoka chuo kikuu cha Marekani katika falme za kiarabu, na ilikua na mada kuu tatu, ambazo ni:

  • - Mtazamo wa maendeleo endelevu katika kuandaa elimu ya maktaba hapa Iraq, iliyo wasilishwa na dokta Khalud Ali Arabi/ kutoka kitengo cha elimu na maktaba/ Juo kikuu cha Mustanswiriyya.
  • - Nafasi ya maktaba katika kutoa maamuzi yatakayo pelekea kufanikiwa kwa mpango wa maendeleo wa Iraq, iliyo wasilishwa na Dokta Salman Judi Daud kutoka chuo kikuu cha Basra/ kitivo cha Adabu/ kitengo cha elimu na maktaba.
  • - Taasisi za elimu za Iraq na changamoto za maendeleo endelevu katika mtazamo wa baadae, iliyo tolewa na Ustadh Jafari Hassan JaasimTwaaiy kutoka katika uongozi wa chuo kikuu cha Diyala/ katibu mkuu wa maktaba kuu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: