Atabatu Abbasiyya tukufu inashiriki katika maonyesho ya vitabu vya dini ya kimataifa ikiwa na zaidi ya aina (300) za vitabu mbalimbali…

Maoni katika picha
Maonyesho ya kitaifa na ya kimataifa, Atabatu Abbasiyya tukufu huchukulia kua ni sehemu muhimu za kujitangaza, imeshiriki katika maonyesho ya vitabu vya dini ya kimataifa awamu ya tano, na maonyesho ya kumi na tatu ya vitabu katika mji mtukufu wa Qum, kupitia tawi lake lililo shehena vitabu mbalimbali, vya kidini na kisekula pamoja na majarida yaliyo beba elimu kubwa, na yanayo lenga watu wa tabaka zote, na kuandikwa kwa lugha rahisi na inayo eleweka, jambo hili ndio linalo fanya wawe na mvuto mkubwa katika maonyesho.

Ushiriki wa maonyesho haya ni miongoni mwa utaratibu wa ushiriki wa maonyesho ya kimataifa. Maonyesho haya sawa na maonyesho mengine, Ataba tukufu imekuja na zaidi ya aina (300) za vitabu vilivyo andikwa, kuhakikiwa na kuchapishwa na Ataba yenyewe, jambo ambalo halipo katika vituo vingine, jambo hili limekua likionyesha utofauti wao na vituo vingine katika maonyesho mengi ya kitaifa na kimataifa ambayo Ataba imeshiriki ikiwa ni pamoja na maonyesho haya.

Kumbuka kua maonyesho ya vitabu vya dini ya mwaka wa tano mfululizo yanafanyika sambamba na maonyesho ya vitabu ya kumi na tatu katika mji mtukufu wa Qum, maonyesho yeto mawili yatafanyika kwa muda wa siku kumi, kuanzia tarehe 15 hadi 25 Februari 2018, kukiwa na jumla ya taasisi na vituo vya usambazaji vinavyo shiriki (376) kutoka Iraq, Sirya, Uturuki, Jodan, Lebanon pamoja na Iran, kuna zaidi ya aina elfu themanini ya vitabu vikiwemo ambavyo vimeonyeshwa kwa mara ya kwanza.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: