Maoni katika picha
Baada ya kutembelea sehemu za chuo na kuangalia selebasi ya masomo inayo tumika, alifurahishwa sana na mpangilio huu wa elimu utakao leta mafanikio makubwa katika elimu ya Iraq hapo baadae.
Katika ziara hii Dokta Alaa Habba alitoa muhadhara unao sema: (Utambuzi wa kiviwanda katika tiba ya sasa na ya baadae) mbele ya rais wa chuo Profesa Jaasim Marzuki na jopo kubwa la walimu na wanafunzi.
Kwa mujibu wa maelezo ya Dokta Alaa Habba: “Muhadhara wake ulichukua saa mbili na alielezea mada ya utambuzi wa kiviwanda katika tiba, hali kadhalika alielezea mambo mbalimbali na akatoa ufafanuzi muhimu kuhusu hali ya sasa na ya baadae katika utambuzi wa kiviwanda, pamoja na kufafanua misamiati muhimu ya kielimu inayo husu walimu wote wa chuo na wanafunzi wao, yenye ujumbe mkubwa unao saidia kukuza uzowefu kielimu na kivitendo”.
Akabainisha kua: “Hakika tunafanya kila tuwezalo kufikisha ujumbe muhimu wa elimu kwa wanafunzi wa chuo cha udaktari hadi katika siku za usoni, na aina ya tiba watakazo toa, kutokana na maendeleo ya kielimu na kiteknolojia katika sekta ya matibabu na vipimo, na upande wa kusoma na kusomesha, mtahitajia teknolojia kubwa na utendaji makini utakao akisi mafanikio ya kielimu na kivitendo”.
Kumbuka kua chuo kikuu cha Ameed ni moja ya taasisi muhimu za elimu zilizo chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu, na kimefungua kitivo cha kwanza cha udaktari chenye kiwango cha kitaifa, na inatumia selebasi ya kimataifa, kwa ajili ya kuhakikisha inafikia viwango bora zaidi kila baada ya muda fulani hufanya kongamano au nadwa za kielimu ambapo hutolewa mihadhara mbalimbali na harakati zingine.