Kumbukumbu ya kifo cha jabali la utekelezaji Ummul Banina (a.s) yafanyika majlisi ya maombolezo katika ukumbi wa haram ya Abulfadhil Abbasi…

Maoni katika picha
Ratiba iliyo andaliwa na Atabatu Abbasiyya tukufu ya kuombolza kifo cha jabali la utekelezaji bibi mtukufu Ummul Banina (a.s) imehusisha vitu vingi, ikiwa ni pamoja na kufanyika kwa majlisi za maombolezo kila siku, kuanzia Ijumaa hadi Juma Pili, hili ni jambo dogo sana ukilinganisha na namna alivyo jitolea bibi huyu mtakasifu katika kuwatangaza Ahlulbait (a.s), kwa kutumia malezi bora na ushujaa wake, na kuienzi nafasi ya malezi katika uislamu, sifa aliyo kua nayo bibi huyu mtukufu, na misimamo yake mizuri ambayo imeshuhudiwa na historia, alikua ni mke wa bwana wetu na Imamu wetu Ali bun Abu Twalib (a.s) na mama wa majemedari wanne walio uawa kwa ajili ya kumlinda ndugu yao bwana wa mashahidi Imamu Hussein (a.s).

Majlisi ilikua inafanywa baada ya swala ya Isha, ilikua inafunguliwa kwa Qur’an tukufu kisha unafuata muhadhara wa kidini kuhusu utukufu na sifa za pekee alizo kua nazo Ummul Banina (a.s), baada ya kumaliza muhadhara ilikua inafanyika majlisi ya matam ikiongozwa na mwimbaji maarufu Mulla Baasim Karbalai, ambaye alikua anaimba kaswida zilizo amsha hisia za mazuwari na kila aliye hudhuria, akielezea utukufu, subira na jihadi aliyo pigana bibi huyu mtukufu katika njia ya Mwenyezi Mungu, kupitia kujitolea watoto wake wanne kwenda kumnusuru Imamu Hussein (a.s).

Kumbuka kua Atabatu Abbasiyya tukufu iliandaa ratiba ya maombolezo iliyo husisha vitu vingi, ikiwa ni pamoja na kutoa mihadhara ya dini, majlisi maalumu za maombolezo, sambamba na kupokea mawakibu (misafara) ya waombolezaji kutoka ndani na nje ya mji mtukufu wa Karbala, wanaokuja kumpa pole Imamu Hussein na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) kutokana na msiba huu.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: