Mada za kihauza na kisekula zinazo husu maudhui za kisasa: kimefanyika kikao cha tatu cha utafiti katika kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu shahada…

Sehemu ya kikao
Imeingia siku mpya miongoni mwa siku za kongamano la kitamaduni na kimataifa Rabiu shahada awamu ya kumi na nne, na kufuatia kumbukumbu ya kuzaliwa kwa Imamu Sajjaad (a.s), asubuhi ya Juma Pili (5 Shabani 1439h) sawa na (22 Aprili 2018m), kimeanza kikao cha tatu cha utafiti ndani ya ukumbi wa Sayyid Auswiyaa katika Atabatu Husseiniyya tukufu, na kuhudhuriwa na kiongozi mkuu wa kisheria Mheshimiwa Shekh Abdulmahdi Karbalai, na katibu wake mkuu Sayyid Jafari Mussawi, pamoja na ujume ulio wakilisha Atabatu Abbasiyya tukufu ukiongozwa na katibu mkuu Mhandisi Muhammad Ashiqar, sambamba na jopo kubwa la wageni wa kongamano kutoka ndani na nje ya Iraq ambao ni wasomi wa dini na sekula, mada zilizo wasilishwa zimekidhi vigezo vya viwango vya tafiti vya kimataifa.

Kikao kilifunguliwa kwa Qur’an tukufu, ahalafu ikasomwa surat Fat-ha kwa ajili ya kuwarehemu mashahidi wa Iraq, na kiliongozwa na Dokta Khaalid Adnaan Hassan, aliye elezea kwa ufupi tafiti tatu za:

  • 1- Dokta Abdulqaadir Yusufu kutoka Lebanon, utafiti wake unasema: (Khutuba za kidini baina ya misimamo mikali na ya kawaida.. khutuba za jihadi kwa mfano).
  • 2- Shekh Fadhili Jazaairiy kutoka Aljeria, utafiti wake unasema: (Kanunu za Mwenyezi Mungu na tatwa tukufu).
  • 3- Dokta Muhammad Na’naa Hassan kutoka Iraq, utafiti wake unasema: (Fatwa iliyo badilisha viwango vya nguvu – utafiti wa athari zake na matokeo yake).

Kikao hiki kilishuhudia umakini wa tafiti ambazo hazijawahi kufanywa hapo kabla, na zilipata mwitikio mkubwa, pia wahudhuriaji walitoa michango yao na maoni yao pamoja na kuuliza maswali, na mwisho watafiti wakapewa zawadi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: