Miongoni mwa ratiba zake za kitamaduni: Madrasa ya Fatuma bint Asadi ya Qur’an yaendesha darsa za kutakasa nafsi…

Maoni katika picha
Miongoni mwa ratiba za kitamaduni zinazo endeshwa na idara ya madrasa za wasichana za Alkafeel katika Atabatu Abbasiyya tukufu, Madrasa ya Fatuma bint Asadi (a.s) ya Qur’an inaendesha darsa za kutakasa nafsi, ambayo ni ratiba ya kimaadili iliyo andaliwa na kamati ya wabobezi inayo lenga tabaka la vijana wa umri tofauti, kwa ajili ya kuwafundisha maadili mema na kuongeza uwelewa wa dini sambamba na kuwafundisha mambo muhimu katika maisha yao chini ya misingi halisi ya kiislamu itokanayo na kitabu cha Mwenyezi Mungu pamoja na hadithi za Mtume na watu wa nyumbani kwake (a.s).

Darsa hizi hufanywa kila wiki kwa muda wa saa tatu katika kituo kikuu cha Swidiqah Twahirah (a.s) kilicho chini ya Atabatu Abbasiyya, darsa hizi zilianza mwanzoni mwa likizo za kiangazi kwa ajili ya kuutumia kwa faida muda wa likizo, zimepata mwitikio mkubwa na washiriki wengi baada ya kutangazwa kwa program hii yenye vipengele vingi vikiwa na lengo la kuandaa kizazi chenye maadili mema ya kiislamu yanayo wawezesha vijana kupambana na changamoto zote za kifikra zinazo lenga kuharibu umma hususan tabaka la vijana, ratiba inamasomo yafuatayo:

  • - Kujifundisha Qur’an usomaji wa tukufu.
  • - Tafsiri ya baadhi za aya za Qur’an zinazo husiana na hali halisi ya maisha ya sasa.
  • - Kusherehesha mambo ya kifiqhi na kiaqida.
  • - Maadili kwa ujumla.
  • - Mihadhara elekezi.
  • - Vipindi vya mapumziko (burudani).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: