Idara ya mawasiliano ya Atabatu Abbasiyya tukufu yasambaza vibanda vya kuelekeza walio patea na walio potelewa na yahimiza kuzingatia maelekezo yake…

Maoni katika picha
Idara ya mawasiliano katika Atabatu Abbasiyya tukufu chini ya kitengo cha miradi imekamilisha uwekaji wa mabanda ya kuelekeza walio potea au kupotelewa, katika maeneo makuu kwenye barabara zinazo elekea Karbala, upande wa mkoa wa Baabil, Najafu na Bagdad, kwa ajili ya kulinda watoto na wazee wasipotee na kama wakipotea waweze kupatikana kwa urahisi, hii inatokana na umuhimu wanaopewa mazuwaru watukufu hususan watoto na wazee wanaokuja katika ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s) kwani wao ni watu muhimu katika ziara hii, ndio sababu kubwa ya kuwekwa mabanda hayo.

Mazuwaru watukufu wamesisitizwa kulipa umuhimu jambo hili, kila banda linamaelfu ya vitambulifo ambavyo vimeandaliwa maalumu kwa ajili ya watoto na wazee, ambavyo vinatakiwa kujazwa jina, mkoa na namba ya simu ya mzazi, mlezi au msimamizi wake, ili iwe rahisi kwa watumishi wa vituo hivi kumpata muhusika kwa haraka na kumtambua mtu atakaye potea kwa urahisi, na kumtangaza katika vituo vyote.

Kumbuka kua mabanda ya kuongoza walio potea na walio potelewa ni miongoni mwa huduma zinazo tolewa na Atabatu Abbasiyya tukufu kwa mazuwaru, katika ziara iliyo pita walifanikiwa kukutanisha maelfu ya watu waliopotea na wasimamizi wao, fahamu kua mabanda haya yanamtandao wa kielektronik ambao una fomu maalumu iliyopo katika mabanda yote, ambayo ikiingizwa taarifa za mtu aliye potea zinaonekana katika mabanda yote.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: