Maahadi ya Qur’ani tukufu yakamilisha maandalizi ya kufungua vituo (200) vya usomaji wa Qur’ani kwa ajili ya mazuwaru wa Arubaini…

Maoni katika picha
Maahadi ya Qur’ani tukufu chini ya kitengo cha maarifa ya kiislamu na kibinadamu cha Atabatu Abbasiyya, imetangaza kukamilika maandalizi ya kufungua vituo (200) vya usomaji wa Qur’ani katika barabara zinazo tumiwa na mazuwaru watukufu kwenda Karbala kufanya ziara ya Arubaini ya Imamu Hussein (a.s), vituo hivyo vitasimamiwa na matawi yake yaliyopo katika mikoa mitatu.

Kwa mujibu wa maelezo ya mkuu wa Maahadi Shekh Jawadi Nasrawi, ambaye aliongeza kua: “Hakika vituo hivyo vitafanya mambo mengi, miongoni mwa mambo hayo ni:




    • 1- Kufundisha usomaji sahihi wa Qur’ani tukufu, hasa sura zinazo somwa mara nyingi katika swala za faradhi za kila siku.




    • 2- Kujibu maswali na kufafanua mambo yanayo husu Qur’ani.




    • 3- Kuendesha kisomo cha Qur’ani tukufu katika kila sehemu ya kituo.




    • 4- Kugawa folda zenye nyaraka zinazo elezea ziara na mambo yanayo husu Qur’ani”.




Akaendelea kusema: “Hakika Maahadi na matawi yake imepanga kuweka vituo hivyo katika mikoa ya Muthanna, Baabil, Najafu pamoja na Karbala tukufu, kwenye barabara kuu zinazo elekea Karbala, miongoni mwa barabara hizo ni: (barabara ya Karbala, Bagdad / Karbala, Baabil / Karbala, Najafu), vituo hivyo vitaendeshwa na wasomi kutoka katika matawi ya Maahadi ya mikoa hiyo, fahamu kua jambo hili linafanywa kwa mwaka wa nne mfululizo kwenye miji hiyo”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: