Picha ya sasa ya Mukhayyamu Husseiniy katika muonekano mpya baada ya upanuzi na ukarabati

Maoni katika picha
Mukhayyamu Husseiniy umeshuhudia upanuzi na ukarabati na kuvaa vazi jipya lililo dariziwa lenye rangi ya kijani na alama za kiislamu za kisasa, zinazo endana na utukufu wake, kamera ya mtandao wa Alkafeel inakuletea picha za jengo hilo katika muonekano wake mpya wa sasa.

Kutokana na maelezo ya wahandisi wa Atabatu Husseiniyya tukufu waliotekeleza mradi huo kwa mtandao wa Alkafeel, mradi huu unasifa zifuatazo:

  • - Eneo lililo ongezwa katika eneo la zamani linaukubwa wa 2m (2215) baada ya kuongeza eneo la shule ya Sajjaad (a.s) iliyo jirani yake.
  • - Kuwekwa paa katika Mukhayyamu Husseiniy yenye ukubwa wa (2m2200).
  • - Mukhayyamu umekua na tabaka tatu kwa ajili ya kupokelea mazuwaru, na unamigahawa miwili, wa wanaume na wanawake, pamoja na eneo la uwanja ndani ya Mukhayyamu.
  • - Mukhayyamu umepauliwa hema tano zenye ukubwa wa (mt10x10), pamoja na hema kubwa mkabala na mlango mkuu wa kuingia, nalo litaitwa hema la Imamu Hussein (a.s).
  • - Mahema yote yamenakshiwa na kuwekwa mapambo mazuri ya dhahabu pamoja na aya za Qur’ani tukufu, kila hema linamadirisha (12) takriban, madirisha ya hema kubwa yanaukubwa wa (mt2).
  • - Limeondolewa dirisha la mbao lililo kuwepo latika hema la Abulfadhil Abbasi (a.s) ndani ya Mukhayyamu Husseiniy na kuwekwa dirisha lililo tengenezwa kwa dhahabu na fedha.
  • - Kupanuliwa sehemu ya mahema manne maalumu ya Imamu Hussein na familia yake, ambayo ni; hema la Imamu Hussein (a.s), hema la Imamu Zainul-Aabidiin (a.s), hema la Hauraa Zainabu (a.s) na hema la Qassim (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: