Kituo kimeweka masharti ya kushiriki katika semina kama yafuatayo:
- 1- Mshiriki awe na umri wa miaka (18 – 35).
- 2- Awe anajua hukumu za Tajwidi (usomaji) na awe anajua aina za sauti.
- 3- Mtihani wa majaribio utafanyika kupitia video ya usomaji wa mshiriki, isiwe imerekodiwa nyuma ya tarehe (28/1/2019).
- 4- Mshiriki anatakiwa kutaja majina yake matatu, mkoa anaotoka na jina la taasisi ambayo yuko chini yake na tarehe ya kuzaliwa kwake pamoja na kutuma picha yake.
- 5- Taasisi itaweka video za washiriki katika ukurasa maalum wa Facebook ya (kituo cha miradi ya Qur’ani) kuna mambo yapasa yazingatiwe wakati wa kurekodi.
Njia na masharti ya kurekodi video:
- 1- Uwe usomaji wa tajwidi unao eleweka na usiokua na makosa.
- 2- Picha isiwekwe vitu vingine vya ziada wala sauti isiongezewe vionjo.
- 3- Picha iwe ya kisasa na irekodiwe rasmi kwa ajili ya kuingia katika semina hii.
- 4- Video isizidi dakika sita.
- 5- Kamera isiwe mbali na msomaji.
- 6- Anatakiwa awe amevaa vizuri wakati wa kujirekodi.
- 7- Viteo zitumwe kwenye telegram kupitia namba hii (07827740369).
- 8- Kila mshiriki atume video moja tu, hairuhusiwi kutuma zaidi ya moja au kubadilisha, atakae fanya hivyo hataruhusiwa kushiriki.
- 9- Sehemu inayo takiwa kusomwa kwenye jaribio ni katika surat Ahzaab (kuanzia aya ya 38/ Maakaana alaa Nnabii…) hadi (aya ya 48/ Wakafaa billahi wakiilaa).
Kuhusu vigezo watakavyo tumia kamati ya majaji ni:
- - Kuangalia hukumu za usomaji (tajwidi, kusimama na kuanza).
- - Mpangilio wa sauti katika usomaji.
- - Naghma katika usomaji.