Majemedari wa kikosi cha Abbasi (a.s) wamemaliza hatua ya kwanza ya safisha safisha katika jangwa la Gharbiyya na wamesisitiza kuwa wataendelea kusaka mabaki ya magaidi wa Daesh…

Maoni katika picha
Uongozi wa kikosi cha Abbasi (a.s) cha wapiganaji umetangaza kumaliza hatua ya kwanza ya kazi za kijeshi, zilizo anza Alfajiri ya Jumapili za kusafisha mabaki ya magaidi katika jangwa la Gharbiyya, wamefikia malengo yote kwa mafanikio makubwa.

Katika ujumbe waliotoa kwa mtandao wa Alkafeel mkuu wa kikosi hicho Ustadh Maitham Zaidi amesema kua: “Hakika wapiganaji wa kikosi ndani ya muda mfupi wamefanikiwa kusafisha kilometa (500) katika jangwa la mji wa Nukhaib kuelekea jangwa la Ramadi, kikosi kimetumia msako wa kasi katika pande zote, pamoja na kumaliza jukumu tulilopangiwa katika hatua ya kwanza, tutaendelea kufanya msako na kuimarisha ulinzi”

Kumbuka kua msako huu unafanywa chini ya usimamizi wa wizara ya ulinzi ya Iraq kwa kuongozwa na kikosi cha mkoa wa Ambaar pamoja na kikosi cha Abbasi (a.s) blugedi ya 26 ya Hashdi Sha’abi, kikosi cha Abbasi kimewakilishwa na blugedi yake namba tano.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: