Dondoo za kumbukumbu: Mwezi pili Rajabu iliangaza nuru ya kumi ya Imamu Ali Haadi (a.s).

Maoni katika picha
Wapenzi na wafuasi wa Maimamu wa Ahlulbait (a.s) siku kama ya leo, mwezi pili Rajabu mwaka wa (212h) –katika riwaya nyingine mwezi kumi na tano Dhul-hijja mwaka wa 214i-, ulizaliwa mwezi wa kumi miongoni mwa miezi ya Muhammadiyya Imamu Ali bun Muhammad bun Ali bun Mussa bun Jafari bun Muhammad bun Ali bun Hussein bun Ali bun Abu Twalib (a.s), katika kijiji cha Baswariyya –kilicho anzishwa na Imamu Mussa bun Jafari (a.s) kipo umbali wa maili tatu kutoka Madina-, Imamu Jawadi (a.s) alimpokea mwanae Ali (a.s) kwa shangwe na furaha kubwa, akamuweka kifuani kwake, akambusu na kumuadhinia katika sikio la kulia kisha akasoma Iqama katika sikio la kushoto, baada ya hapo akataja jina alilo chaguliwa kutoka mbinguni la (Ali) na akampa jina lakunia la baba Hassan (Abul-Hassan), likiwa ni jina la kurithi kwa babu yake Ali bun Abu Twalib baba Hassa (a.s), kwa ajili ya kupambanua baina ya Abul Hassan Ridhwa na Abul Hassan kiongozi wa waumini katika jina lake imeongezwa (wa tatu), kwa hiyo anaitwa, Ali Haadi Abul Hassan wa tatu (a.s).

Mama yake anaitwa Ummul Waladu, inasemekana jina lake ni Sumana, vilevile huitwa Sumana wa Moroko.

Majina yake ya sifa (laqabu), anamajina mengi, miongoni mwake ni: Murtadhwa, Haadi, Askariy, Aalimu, Dalilu, Muwadhihu, Rashidu, Shahidu, Wafiyyu, Najibu, Mutaqi, Mutawakilu, Khaalisu, Naaswihu, Fataahu, Naqiyyu, Faqiihu, Amiinu, Twayyib, majina maarufu zaidi ni Haadi na Naqiyyu.

Majina yake ya kuniyya, anaitwa: (Abul Hassan) na huitwa Abul hassan wa tatu.

Nafasi yake kielimu (a.s):

Mabingwa wa historia wamekubaliana kua Imamu (a.s) alikua na elimu kubwa sana kushinda wanachuoni wote wa zama zake, Shekh Tusi katika kitabu chake cha (Rijalu Tusi) ameandika majina ya watu mia moja themanini na tano waliosoma na kupokea hadithi kutoka kwake.

Alikua kimbilio la wasomi wa Fiqhi na Sheria, alikua chimbuko la vitabu vya hadithi, mijadala, fiqhi, tafsiri na vinginevyo kutokana na mafundisho yake.

Miongoni wa mafundisho ya Imamu Haadi (a.s):

  • 1- Amesema (a.s): “Atakaye ridhia nafsi yake wengi watamchukia”.
  • 2- Anasema (a.s): “Msiba wa mwenye subira ni mmoja na asiyekua na subira ni miwili”.
  • 3- Anasema (a.s): “Uzembe ni chaguo la wapumbavu na kazi ya wajinga”.
  • 4- Anasema (a.s): “Kusinzia ni kutamu kushina kulala na njaa huongeza uzuri wa chakula”.
  • 5- Anasema (a.s): “Taja kifo chako kwa familia yako hakuna mganga wala mpenzi atakaekufaa”.
  • 6- Anasema (a.s): “Makadirio hukuonyesha usiyotarajia katika akili yako”.
  • 7- Anasema (a.s): “Hekima haionekani katika mazingira ya ufisadi”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: