Mgahawa wa Atabatu Abbasiyya tukufu unagawa mamia ya sahani za chakula kwa waombolezaji wa kifo cha Imamu Haadi (a.s).

Maoni katika picha
Kila mtu anajua kua siku ya tatu ya mwezi wa Rajabu makundi makubwa ya mazuwaru huelekea katika mji mtukufu wa Samaraa, kuhuisha kumbukumbu ya kifo cha Imamu wa kumi, Imamu Ali Haadi (a.s) pembezoni mwa kaburi lake takatifu, vile vile kundi lingine kubwa halikuweza kwenda Samaraa kwa sababu tofauti, kuna ambao wamekosa nafasi, wengine wako mbali na mji huo, na wengine huenda katika mji mtukufu wa Karbala na kutembelea kaburi la bwana wa mashahidi na ndugu yake Abulfadhil Abbasi (a.s) kama sehemu ya kuomboleza msiba huu mchungu.

Atabatu Abbasiyya tukufu kupitia mgahawa (mudhifu) wa Abulfadhil Abbasi (a.s), ikiwa ni katika utaratibu wake maalumu katika kuomboleza vifo vya watu wa nyumba ya Mtume (a.s), imegawa mamia ya sahani za chakula kwa mazuwaru waliokuja katika mji wa Karbala kuomboleza kifo cha Imamu Ali Haadi (a.s), kwa kutumia madirisha ya kugawa chakula ya nje.

Fahamu kua makundi makubwa ya waumini –pamoja na mawakibu za waombolezaji- kutoka Karbala na miji jirani, katika siku kama ya leo huja kwenye kaburi la Abu Abdillahi Hussein na ndugu yake mbeba bendera wake Abulfadhil Abbasi (a.s), kwa ajili ya kuhuisha kumbukumbu ya kifo cha Imamu Ali Haadi (a.s).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: