Ugeni kutoka umoja wa Ulaya kupitia mradi wa (WALADU) unatembelea makumbusho ya Alkafeel na umeonyesha kufurahishwa na walicho kiona katika makumbusho hayo.

Maoni katika picha
Ugeni kutoka umoja wa Ulaya katika mradi wa (WALADU) ambao ni mradi wa wabobezi wa historia na mambo ya kale, wameonyesha kufurahishwa na mambo yaliyomo katika makumbusho ya Alkafeel ya vitu na nakala kale, sambamba na kuridhishwa na kazi nzuri inayo fanywa na wahudumu wa makumbusho hiyo, kuanzia namna walivyo pangilia vitu pamoja na namna vinavyo tunzwa.

Yametokea hayo katika ziara iliyo fanywa na ugeni huo na kuongozwa na Profesa CIGDEM MAER kutoka chuo kikuu cha Bolina Italia na chuo kikuu cha Kotesh cha Istambul Uturuki, wametembelea makumbusho hiyo huku wakisindikizwa na rais wa makumbusho Ustadh Swadiq Laazim, wageni wasikiliza maelezo kwa ufupi kuhusu makumbusho na njia ya uhifadhi wa vifaa vyake, pia wametembelea ukumbi wa maonyesho ya vifaa vilivyopo katika makumbusho, pamoja na kupewa maelezo kwa kifupi kuhusu kila kifaa.

Mwishoni mwa ziara yao Pr. CIGDEM MANER Alionyesha kuridhiswa kwake na alicho kiona katika makumbusho hiyo, akasema: “Nawapongeza sana kutokana na makumbusho hii ya kimataifa” akasisitiza kua: “Hakika hii ni makumbusho kubwa na inavitu vingi vya thamani”.

Baada ya hapo ugeni ulikwenda kukutana na kiongozi mkuu wa kisheria katika Atabatu Abbasiyya tukufu Sayyid Ahmadi Swafi, wakajadili mambo mbalimbali kuhusu uzowefu wao katika mambo ya makumbusho na kuhusu wanafunzi wa Alkafeel wanao somea mambo ya makumbusho.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: