Ugeni kutoka kitengo cha Dini unashiriki katika hafla ya kuwazawadia mabinti waliofikisha umri wa kuwajibikiwa na sharia katika wilaya ya Swawira.

Maoni katika picha
Atabatu Abbasiyya tukufu imetuma wajumbe katika hafla ya kuwazawadia mabinti waliofikisha umri wa kuwajibikiwa na sharia katika wilaya ya Swawira mkoani Waasit, imewakilishwa na watumishi kutoka kitengo cha Dini kwenye hafla hiyo iliyo fanyika ndani ya kituo cha Imamu Msubiriwa (a.s), hafla imehudhuriwa na vingozi wengi wa Dini pamoja na mabint hao na wazazi wao.

Mjumbe katika wageni wa Ataba, Shekh Muhsin Asadiy amesema kua: “Hakika ni fursa nzuri ya kushirikiana na binti zetu wa wilaya ya Swawira katika hafla hii, kutokana na umuhimu wa umri wa kubalekhe kwa wasichana na wavulana, huu ni umri muhimu sana katika uhai wao, wamejiandaa vipi kimwili na kiakili katika kukabiliana na mabadiliko makubwa na muhimu katika uhai wao, mabadiliko ya kutoka katika hatua ya utoto na kuingia katika hatua ya ukubwa, hatua ya makuzi na mitihani katika maisha, hafla hii ni uzinduzi kwa kila kijana wa kumtaka awajibike katika kutekeleza majukumu aliyo pewa katika maisha yake”.

Akaongeza kua: “Tuliandaa zawadi za mabinti ambao walikua zaidi ya mia moja, wamepewa vitambaa vya kutabaruku na malalo ya Abulfadhil Abbasi pamoja na vipeperushi vya mafundisho na maelekezo mbalimbali yanayo endana na umri wao wa sasa na siku zijazo”.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: