Katika mazingira tulivu ya kiimani ndani ya haram tukufu ya kaburi la mnyweshaji wenye kiu Karbala Abulfadhil Abbasi (a.s), malalo imefurika mazuwaru kutoka ndani na nje ya mkoa wa Karbala, hii ndio kawaida katika kila usiku wa Ijumaa.
Kutokana na wingi wa mazuwaru, watumishi wa Abulfadhil Abbasi wamefanya kila wawezalo katika kuwahudumia na kuhakikisha wanafanya ziara na ibada kwa Amani na utulivu.
Mazuwaru walipokua wakiomba haja zao wametanguliza zaidi kuliombea amani taifa la Iraq na raia wake pamoja na kuwalinda wapiganaji wanaojitolea kwa ajili ya taifa hili.
Kamera ya mtandao wa Alkafeel imeshuhudia mazingira ya ziara hiyo na inakuletea baadhi ya picha..