Mwendelezo wa uenzi wa mabweni ya chuo kikuu cha Al-Ameed chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu.

Maoni katika picha
Kitengo cha uhandisi cha Atabatu Abbasiyya tukufu kinaendelea na hatua ya pili ya ujenzi wa bweni (nyumba za wanafunzi) za chuo kikuu cha Al-Ameed, kazi hiyo ilianza tangu mwezi wa Desemba (2018m), ikafanywa kwa miezi mitatu mfululizo, katika hatua ya kwanza lilijengwa ghorofa la kwanza na la pilli, na katika hatua hii tunajenga ghorofa la tatu na la nne.

Kuhusu mradi huu tumeongea na Mhandisi Alaa Hussein kutoka kitengo cha usimamizi wa kihandisi amesema kua: “Tumeanza kazi ya ujenzi katika hatua tofauti, tumeanza kwa kuweka nguzo kwa kutumua vifaa vya chuma vilivyo tengenezwa na kitengo cha uhandisi, baada ya kuweka nguzo tukazisakafia kwa block, halafu tukaziwekea mfumo wa umeme na mawasiliano”.

Akaongeza kua: “Muda wa kazi uliopangwa kwa kila ghorofa ni miezi mitatu, kwa kufanya kazi kila siku saa (24), idara zoto zilizo chini ya usimamizi wa kihandisi zinashiriki katika ujenzi huu, zikiongozwa na idara ya majengo ya nje”.

Fahamu kua kitengo cha usimamizi wa kihandisi cha Atabatu Abbasiyya tukufu kina nafasi kubwa katika ujenzi wa majengo mengi ambayo yapo chini ya Atabatu Abbasiyya tukufu ndani na nje ya Ataba, kina mafundi mahiri wenye uzowefu mkubwa wa aina zote za ujenzi.
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: