Msafara wa Alwafaa unaotoa huduma za kibinaadamu unaelekea katika mji wa Samawah

Maoni katika picha
Asubuhi ya Jumamosi (29 Rajabu 1440h) sawa na (6 April 2019m) msafara wa Alwafaa umeanza safari ya kuelekea Samawah katika mkoa wa Muthanna, ukiwa na gari zaidi ya (350) zilizo beba vitu mbalimbali, kwa ajili ya kusaidia: (familia za mashahidi wa Hashdi Sha’abi na wanajeshi wa serikali, majeruhi wa vita tukufu ya kujilinda, mayatima na familia zenye maisha magumu), vitu walivyo beba ni: (vyakula, dawa, mahitaji muhimu ya kimaisha pamoja na hela), msafara huo utachukua siku tatu na utaangalia jinsi ya kutoa msaada wa kihandisi katika mkoa huo kulingana na mahitaji ya sasa.

Msafara huu ni sehemu ya mfululizo wa misafara ya aina hii inayo fanywa katika mikoa mingine ya Iraq chini ya uratibu wa uongozi mkuu wa Atabatu Abbasiyya tukufu na utekelezaji wa viongozi wa kikosi cha Abbasi (a.s) cha wapiganaji blugedi ya 26 katika Hashdi Sha’abi, kwa kutumia (mawakibu za kutoa misaada na idara za ustawi wa jamii katika mikoa 13 – ofisi kuu ya msafara wa Alwafaa- wawakilishi wa kikosi cha Abbasi, taasisi za kiraia zinazo toa huduma za kibinaadamu – pamoja na wahisani wengine), pamoja na kuwasiliana na: (serikali ya mkoa wa Muthanna, na mwakilishi wa Marjaa Dini mkuu katika mji wa Najafu, na idara ya ustawi wa jamii ya Samawah, wawakilishi wa kikosi cha Abbasi (a.s) waliopo katika mji wa Samawah, pamoja na taasisi zingine za kiraia).
Maoni ya wasomaji
Hakuna maoni
Kuweka maoni
Jina:
Nchi:
Barua pepe:
Kushiriki: